Saturday, April 27, 2013

PPF YATOA ZAWADI ZA KOMPYUTA MPAKATO KWA WANAFUNZI 14 KATIKA HALFA YA KUTIMIZA MIAKA 10 YA FAO LA ELIMU LINALOTOLEWA NA MFUKO WA PENSHENI PPF.


Wanafunzi wapatao 14  leo wamezawadiwa kompyuta mpakato /laptop katika halfa ya chakula chamchana kilichoandaliwa  kuadhimisha miaka 10 ya fao la Elimu  iliyofanyika  katika ukumbi wa mwalimu Nyerere Dar es salaam.na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa serikali kama waziri wa kazi na ajira mhe.Gaudensia Kabaka,Naibu waziri wa fedha  mhe. Saada Mkuya Salum,Naibu waziri wa katiba  na sheria  mhe;Anjelina Kairuki,mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  Mhe.Said Mecky Sadiki,Naibu  katibu  mkuu was  maendeleo ya jamii ,jinsia na watoto Bi. Anna Maembe,kamishna wa elimu  profesa .Eustella Bhalalusesa mkurugenzi  mkuu wa  mamlaka  ya usimamizi  wa sekta  ya hifadhi  ya jamii ( SSRA) ,Ndugu  Irene Isaka na wengine wengi.

 Wanafunzi hao  walizawadiwa zawadi hizo na mgeni rasmi mama Salma kikwete,ambaye amepongeza mfuko wa pensheni PPF  kwa kuanzia fao hilo kwani  kwa mwaka jana pekee waliweza kusomesha wanafunzi zaidi ya 1333 katika shule mbali mbali za msingi na sekondari hapa nchini Tanzania bara na  visiwani.

Watoto wanaofadhiliwa na mfuko wa pensheni wa PPF ni watoto ambao wamepoteza mzazi  kati ya baba au mama na mwanachama awe ameshachangia mfuko kwa zaidi ya miaka 3 au zaidi , na mwanafunzi atapata fursa ya kusomeshwa kwa kulipiwa karo na mahitaji mengine kama  sare za shule vifaa( stationeries)usafiri, chakula kwa kuzingatia  mshahara wa mzazi aliyekuwa mwanachama  wa PPF na watoto wanasomeshwa kuanzia  awali( chekechea ) hadi kidato cha nne na pia wasizidi watoto wanne..

 Nae mkurugenzi mkuu wa mfuko wa pensheni  wa PPF bwana Wiliam Erio ameelezea mafanikio makubwa ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978 na kusema kuwa mapato ya shirika hilo yameongezeka kila mwaka ,hii imewezesha  thamani ya mfuko kufikia shilingi trilioni moja nukta sifuri kenda (1.09)mwezi desemba mwaka 2012.

Aidha mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya mfuko wa pensheni wa PPF  proffesa  Adolf Faustine Mkenda  katika hafla hiyo aliweza kuelezea changamoto 3  zinazokabila fao hilo la elimu kuwa ni baaadhi ya shule kutotuma taarifa za mitihani za wanafunzi wanaosomeshwa na fao hilo.

Changamoto nyingine inayokabili fao hilo ni udhibitisho wa uhakika kuwa wanaosomeshwa ni wale wanaostaiki na sio watoto wengine,na changamoto  nyingine ni waajiri kuchelewa kutuma taarifa za vifo vya wafanyakazi mara wanapofariki hivyo wanafunzi hupata usumbufu wa kuchelewa kulipiwa karo hususan kifo kinapotokea wakati wa mwanzo wa masomo hivyo huadhiri maendeleo ya mwanafunzi.

Ombi la mgeni rasmi kwa mfuko wa pensheni wa PPF ni kuangalia kama hali itaruhusu waweze kuongeza ,kipindi cha kusomesha kutoka  kidato cha nne hadi kidato cha sita  ili kumuwezesha mwanafunzi kuweza kufikia malengo ya kielimu kuliko kumsomesha mpaka kidato cha nne elimu amabyo haitamruhusu  kuendelea kusoma ,pia amependekeza na kuomba hivyo akijua fika kuwa kama mwanafunzi atasomeshwa mpaka kidato cha sita basi ataweza kuendelea na chuo kikuu kwa kuwa vyuo vikuu vinatoa  mkopo kwa wanafunzi.

Mwisho mgeni rasmi mama salma kikwete aliwaasa wanafunzi waliofanya vizuri na kuzawadiwa kompyuta mpakato kutumia kwa matumizi sahihi na ya kielimu zaidi na sio kwa vitendo vya kuvunja maadili na kupotosha maadili katika jamii.

No comments:

Post a Comment