Tuesday, July 2, 2013

BYE BYE BARACK NA MICHELLE OBAMA TUTAONANA TENA KARIBUNI TENA TANZANIA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Barack Obama  wakipokea saluti wakati nyimbo za Taifa zikipigwa ,wakati  wa kuondoka kwa Rais huyo wa Marekani  leo katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julias Nyerere .
Nyuma yao ni mama Salma Kikwete  na mama Michelle Obama pamoja na mkuu wa majeshi Davis Mamunyange  pamoja na IGP Said Mwema .
Kushoto ni mkuu wa itifaki  Balozi Mohamed Maharage na mkuu wa itifaki wa ikulu ya  Marekani ( white House ) balozi  capricia Marshall..Ziara ya  Rais Obama inatajwa kuwa  moja kati ya  ziara za viongozi wan je zilifanikiwa sana, ambapo pia maelfu ya Watanaznia waljitokeza kumlaki na kumuaga.
Rais Barack Obama akiagama na mstahiki  Meya wa jiji la Dar es salaam huku Mstahiki Meya  wa Ilala pamojana Balozi wa Tanzania nchini Marekani mhe.Liberata Mulamula wakisubiria zamu zao za kuagana na Rais wa Marekani.
HAOOO  Rais Obama  na mkewe wakikwea pipa lao la Air Force One tayari kwa safari ya kurudi nchini Marekani mara baada ya kumaliza ziara ya siku Mbili nchini TANZANIA.

Rais Obama na mkewe wakiwapungua  mikono kuwaaga watanzania waliofika katika uwanja wa ndege kuwasindikiza kwa safari yao .
Rais kikwete na mama Salma  Kikwete wakiagana na wageni wao katika uwanja wa kimataifa wa mwalimu Julias Nyerere leo .

Rais Kikwete ,Mama  Salma na Kikwete,Naibu Waziri wa kilimo mhe  Adam Malima (kushoto),Mkuu wa Mkoa  wa  Dar es salaam ,balozi  wa Marekani hapa nchini Mhe.Alfonso lenhardt  wakiwapungia  mikono kuwaaga wageni wao  ambao wamemaliza  ziara yao ya siku mbili hapa nchini Tanzania baada ya k ufika  jana na kufika ikulu kisha kuongea na Rais wa Tanzania Mhe.DKT  JAKAYA KIKWETE na baada ya hapo alipata fursa ya kuongea na waandishi wahabari .

Pia Rais Barack Obama  alipata wasaa wa kuzindua barabara iliyotambulika kama OCEAN ROAD hapo awali na Jana kubatizwa na kupewa jina jipya la BARACK  OBAMA DRIVE ,
Pia kwa siku ya leo Rais Obama aliweza kutembelea kinu cha kufua umeme cha symbion  kilichopo  Ubungo Tanesco karibu kabisa na  kituo maraarufu cha daladala cha Ubungo .

No comments:

Post a Comment