Tuesday, February 25, 2014

HERO DAWN AINA MPYA YA PIKIPIKI ILIYOZINDULIWA NCHINI TANZANIA


Baadhi ya wananchi wakipata maelekezo kutoka kwa mwakilishi wa Kampuni ya Astarc Group wakati wa uzinduzi wa aina mpya ya Pikipiki ijulikanayo kwa jina la Hero Dawn leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Eliphace Marwa - Maelezo)
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa aina mpya ya Pikipiki ijulikanayo kwa jina la Hero Dawn Bw. Subhash Patel (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Pikipiki hizo zinazotengenezwa na kusambazwa na kampuni ya Astarc Group leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Astarc Group Bw.Salil Musale na kulia ni Mkurugenzi wa Astarc Group Africa Bw. Sameer Musale.
Subhash Patel ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Pikipiki mpya aina ya Hero Dawn akijaribu moja ya pikipiki aina ya Hero Karizma inayotengenezwa na kusambazwa na kampuni ya Astarc Group
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa aina mpya ya Pikipiki ijulikanayo kwa jina la Hero Dawn Bw. Subhash Patel (kushoto) akiteta jambo na Afisa Uhusiano wa kampuni ya Astarc Group Bw. Mukesh Joshi  leo jijini Dar es Salaam. kulia ni Mkurugenzi wa Astarc Group Africa Bw. Sameer Musale
Mkurugenzi wa Astarc Group Africa Bw. Sameer Musale akitoa historia fupi ya kampuni ya Astarc ambayo ni watengenezaji na wasambazajiwa pikipiki aina ya Hero ambazo zimezinduliwa leo jijini Dar es Salaam. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni ya Astarc Group akimkaribisha mgeni rasmi Bw, Subhash Patel (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa aina mpya ya pikipiki ijulikanayo kwa jina la Hero Dawn.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa aina mpya ya pikipiki Hero Dawn Bw. Subhash Patel akizungumza na waaandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa aina mpya ya pikipiki ijulikanayo kwa jina la Hero Dawn(Pesa zaidi mfukoni) mapema leo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Astarc Group Bw.Salil Musale akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa aina mpya ya pikipiki ijulikanayo kwa jina la Hero Dawn (Pesa zaidi mfukoni) mapema leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wananchi wakijibu maswali mbalimbali kuhusu pikipiki aina ya Hero Dawn wakati wa uzinduzi wa pikipiki hiyo leo jijini Dar es Salaam. 
Mgeni rasmi, Subhash Patel pamoja na uongozi wa kampuni hiyo, wakifurahia uzinduzi huo.

No comments:

Post a Comment