Thursday, February 27, 2014

TUZO MPYA ZA USHAIRI ZAZINDULIWA ZITAHUSISHA MASHAIRI YA AINA ZOTE HIP HOP,TAARABU NA MASHAIRI MENGINE YA KIMAPOKEO NA TUNGO HURU

 kamati ya usimamizi  wa tuzo ya Ibrahim Hussein wakiwa tayari katika ukumbi wa habari maelezo kabla ya kutangaza rasmi kuzinduliwa kwa tuzo ya ushairi itakayo husisha nyimbo za mashairi ,taarabu na  muziki wa kizazi kipya yaani hip hop.
 Mwenyekiti kamati ya kusimamia Tuzo  ya mashairi ya Ibrahim Hussein akizindua rasmi  na kutangaza kuanza  kwa tuzo hizo katika ukumbi wa habari maelezo
 proffesa mstaafu TATAKI-CKI-PROFFESA MUGYABUSO MULOKOZI akifafanua jambo alipokuwa katika mkutano na waandhishi wa habari katika ukumbi wa habari maelezo juu ya kuishiriki katika tuzo za profesa Ebrahim Hussein ,wakifuatilia kutangazwa kwa kuzinduliwa kwa  tuzo mpya za maishairi na nyimbo (picha zote na Gasper Sambweti  wa www.http://sambweti.blogspot.com)
  Baadhi ya waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali wakifuatilia kutangazwa kwa kuzinduliwa kwa  tuzo mpya za maishairi na nyimbo (picha zote na Gasper Sambweti  wa www.http://sambweti.blogspot.com)
  Baadhi ya waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali wakifuatilia kutangazwa kwa kuzinduliwa kwa  tuzo mpya za maishairi na nyimbo (picha zote na Gasper Sambweti  wa www.http://sambweti.blogspot.com)
  Baadhi ya waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali wakifuatilia kutangazwa kwa kuzinduliwa kwa  tuzo mpya za maishairi na nyimbo (picha zote na Gasper Sambweti  wa www.http://sambweti.blogspot.com)
 Baadhi ya waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali wakifuatilia kutangazwa kwa kuzinduliwa kwa  tuzo mpya za maishairi na nyimbo (picha zote na Gasper Sambweti  wa www.http://sambweti.blogspot.com)
PICHA JUU NI MTUNZI NA MSHAIRI GERALD BELKIN
    
PICHA JUU NI MTUNZI NA MSHAIRI PROFESSA EBRHIM HUSEIN 

Kamati ya usimamizi  wa Tunzo ya Ushairi ya Ebrahim Hussein ,kwa kushirikia
na na Tanzania Gatsby  Trust (TGT) na Mkuki na Nyota Publishers ,inapenda kutangaza kwa umma uzinduzi wa shindano jipya la ushairi
Lengo kuu la shindano hili ni kumkumbuka mwanzilishi wa Tunzo  hii ,Marehemu Geralnada Belkin,mpiga filamu wa Canada aliyeishi Tanzania  katika miaka ya 1970 .Bwana Belkini aliipenda lugha na fasihi ya Kiswahili naalifanya kazi na mtunzi Ebrahim Hussein kuikuza.Alichangia  mfuko akitaka uwe chachu ya kuendeleza Kiswahili,hasa utunzi wa mashairi.TGT ,shirika linalosimamia  mfuko huu ,imewashirikisha  wajumbe  wa kamati kutoka Mkuki na Nyota Publishers pamoja na wanazuoni mbali mbali wa ushairi katika  kuendesha  shindano hili lililofunguliwa rasmi leo tarehe 26/02/2014

MALENGO MAKUBWA YA SHINDANO HILI.
·        Kuuenzi mchango wa mtunzi,mwanafasihi ,mwanatamthilia ,mtengeneza filamu na mwalimu  mashauri TANZNAIA proffesa Ebrahim Hussein
·        Kukuza fasihi na lugha ya Kiswahili  kwa kuibua  na  vipaji  vya watunzi  wa mashairi na nyimbo
·         
·        Kuongeza idadi ya maandikabla ya mwezi augustshi ya bora katika hazina ya vitabu vya Kiswahilili .
 la majaji limeundwa kwa ajili ya kupitia tungo na kuhagua washindi.Majaji wataalam wa lugh ya Kiswahili  na ushairi,wakiwamo waalimu wa fasihi,wataongozwa na misingi ya kutokuwa na upendeleo.vijana na washair wa tungo za iana mbali mbali (ya kijadi,ya kisiasa )wanakaribishwa kushiriki kila mmoja bila kujali umri ,jinsia ,kazi dini na ulemavu au mnahali anapotoka anakaribishwa kushiriki katika shindano hili.
Shindano litafunguliwa 30 mei 2014 ,na washindi watatangazwa kabla ya mwezi Agosti ,Mshindi wa kwanza atapata zawadi ya shilingi 2000,000?= mshindi wa pili  Atapata 1300000/=  na watatu 70000/=

Melezo ya tunzo hii
1.hili ni shindano la ushairi katikaq lugha ya KISWAHILI
2.Kwa mwaka Huuu tungo zitakazo shirikiahwa ni aina mbili  tu:maishairi na Nyimbo
 MASHAIRI
Yanaweza kuwa:
a)Ya kimapokeo  yenye kuzingatia kanuni na urari wa vina na mizani kama zilivyofafanuliwa na Amri Abedi na wataalam wengine AU
b)Mashairi Huru (masivina)yasiyozingatia kanuni za urari wa vina na mizani

2.2 NYIMBO
a) Zinaweza kuwa kimapokeo zenye kuzingatia  kanuni za bahari ya wimbo katika ushairi  wa kiswahili (k.m. zile za taarabu)
b)Za kizazi kipya “(mathalani zile za hip hop,bongo fleva )
MUHIMU ; Tenzi /Tendi hazitahusika katika shindano  hili,Aidha  ,kazi za kinathari ,kama riwaya au tamthilia ,hazitahusika.
3.0 VIGEZO
Kila mshiriki awasilishe mswada MMOJA tu wenye tungo TATU tu,mswada wenye Tungo Zaidi ya tatu hutashughulikiwa  wala kushindanishwa.
3.1 Tungo ziwe ni za mtunzi mwenyewe ,zisiigwe au kunakiliwa  kutoka kwa mtunzi au watunzi wengine.

3.2 Tungo ziwe mpya kabisa .yaani ,zisiwe zimepata kuchapishwa katika magazeti  ,magazine,majarida au vitabuni ,kutiwa  katika CD au kanda kucheza jukwaani, redion  au kutangaIzwa  na kusambazwa  kupitia  katika mitandao


3.3 Kila Utungo wa kimapokea uzingatie  kanuni za kijadi  za utunzi ,na usipungue  beti 10 au kuzidi 15.
3.4 Utungo wa wimbo ,pamoja kuzingatia kanuni zinazohusika ,usipungue beti 3 wala kuzidi beti  10
3.5 Utungo huru  usipungue  mishororo(mistari )3 wala kuzidi  mishororo 50.
3.6 Mtunzi  atachagua  mwenyewe  mada na maudhui  ya utungo wake.
3.7 Tungo ziheshimu miiko ya kijamii na kimaadili
4.0  VIGEZO VYA USHINDI
JOPO LA WAAMUZI LITAZINGATIA VIGEZO VIFUATAVYO:
1)Usaili:Ni kazi ya mtunzi mwenyewe?
2)Lugha na mtindo :Ufasaha na upekee
3)Uzingativu wa  kanuni  za bahari /aina ya utungo inayohusika
4)Uzito wa fikra na maudhui ,na usadifu  wake kwa jamii
5)Mguso na hisia ,na mvuto kwa msomaji

No comments:

Post a Comment