Tuesday, March 18, 2014

Ole Sendeka, Lekule Laiza wamfagilia Ridhwani Kikwete Chalinze

*Wawataka wananchi wa Chalinze wamchague Ridhwani Kikwete

Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Jakaya Kikwete, akiwa katika Mkutano na Wazee wa Kimasai walipokuwa wakijadilina juu ya suala la Wafugaji wa Chalinze na Pwani kwa Ujumla,jana Machi 17,2014 kwenye Ukumbi wa Masai,Chalinze

Mbunge wa Jimbo la Simanjiro, Christopher Ole Sendeka akiwaomba Wananchi wa Lugoba, Jimbo la Chalinze kutofanya makosa kwenye Uchaguzi Mdogo ndani ya Jimbo lao na Wampigie Kura, Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Jakaya Kikwete. Sendeka aliyasema hayo jana Machi 17,2014 katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Sokoni wakati alipopita kuwasalimia WanaChalinze
Mbunge wa Jimbo la Longido, Lekule Laiza akiwasalimia Wana Chalinze.
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akipokea moja ya kati ya Kadi mbili za Chadema kutoka kwa aliekuwa Mwanachama wa Chadema,Mrisho Issa mkazi wa Kijiji cha Msata,ndani ya Jimbo la Chalinze.Mwingine alierudisha kadi ni Kassim Msakamali (hayupo pichani)
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete (katikati) akiwainua mikono Wanachama wapya wa Chama cha Mapinduzi,Kassim Msakamali (wa pili kushoto) na Mrisho Issa (wa pili kulia) ambao wote ni Wananchi wa Kijiji cha Msata, Chalinze.Kulia ni Meneja wa Kampeni za Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM), Steven Kazidi.
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Jakaya Kikwete (aliesimama kulia) akizungumza machache wakati alipofika kuhani msiba wa Mtoto wa Mzee Mashaka Athuman mkazi wa kijiji cha Rupungwi,Kata ya Mandela iliopo ndani ya Jimbo la Chalinze jana   
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Jakaya Kikwete aiwasalimia wananchi wa Lugoba, Chalinze.
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwa amekabidhiwa fimbo ikiwa ni ishara ya kusimikwa na kuwa Laigwanani wa Kimasai na Laigwanan Ole Masingijana . (Picha zote na Othman Michuzi) 

No comments:

Post a Comment