Thursday, July 31, 2014

Monusco na majeshi ya DRC yadhibiti vijiji Kivu


Vikosi vya Kulinda Amani vya Umoja wa Mataifa vikishirikiana na vikosi vya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo vimefanikiwa kuvikomboa vijiji 20 vilivyokuwa vikidhibitiwa na makundi ya wanamgambo wanaobeba silaha mashariki mwa nchi hiyo. Luteni Kanali Felix Prosper Basse Msemaji wa Monusco amesema leo kuwa, majeshi ya Kongo yakiendesha operesheni ya pamoja na Monusco yamefanikiwa kuvidhibiti vijiji hivyo vilivyoko katika maeneo ya Beni na Libero katika jimbo la Kivu Kaskazini. Luteni Kanali Basse amesema kuwa, operesheni hiyo ya pamoja ya kijeshi imefanyika kwa lengo la kukomesha mauaji, unyanyasaji, ubakaji, uporaji na utumikishaji watoto kwenye makundi hayo ya waasi. Operesheni  katika mji wa Beni ilililenga kundi la waasi wa Uganda wa ADF/NALU walioko mashariki mwa Kongo. 

No comments:

Post a Comment