Monday, August 25, 2014

MIGA katika nchi za Afrika Kusini mwa Sahara





MIGA TAARIFA KWA MUHTASARI

Afrika Kusini mwa Sahara


                                                                                                                                                                                                                                                                     KUDHAMINI UWEKEZAJI   KUHAKIKISHA FURSA




  Bara linalopiga Hatua
Nchi za Bara la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara zimeendelea kuwa eneo linalo wavutia wawekezaji. Nchi hizi zimeshuhudia kuongezeka kwa kiwango cha juu na endelevu katika ukuaji wa uchumi katika miaka ya hivi karibuni, wakati makadirio yakionyesha kupanuka kwa uchumi kwa asilimia 5 kwa mwaka   2012, ikifuatia kupanuka kwingine kwa kiwango cha asilimia 4.7 mwaka 2011. Wakati sekta ya madini imekuwa ndio msukumo mkuu wa uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja katika bara hili, uwekezaji katika sekta ambazo si za uziduzi pia umekuwa ukiongezeka kutokana na maboresho ya taasisi za udhibiti, utawala bora na kwa ujumla mazingira mazuri ya kufanya biashara katika kanda hii—pia kuongezeka kwa tabaka la kati ambalo huvutia wawekezaji wanaotafuta masoko mapya.

Hisia za Hatari za Kisiasa Hukwamisha Uwekezaji uHH
Licha ya uwezo wake mkubwa, gharama za chini za nguvu kazi, na maliasili nyingi, wawekezaji wengi bado wanakuwa na wasiwasi wa kuwekeza katika bara la Afrika. Bara hili ni eneo lililo na nchi 17 ambazo Benki ya Dunia huzianisha kuwa ni nchi “tete na zilizogubikwa na migogoro”. Kwa baadhi ya wawekezaji, hatari za kufanya biashara katika nchi zilizo na usalama mdogo kisiasa mara nyingi ni kubwa zaidi kuliko faida ya kuingia masoko yenye faida kubwa. Na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara bado zinaonekana kuwa zina hatari kubwa, zenye gharama kubwa ya kufanya biashara. Hatari ambazo zinawapa wasiwasi wawekezaji na wakopeshaji mara nyingi zinahusiana na imani ndogo katika mfumo wa mahakama  

na taasisi za udhibiti, utawala mbovu, rushwa na uhaba wa utawala wa sheria, kutokuwepo kwa usimamizi wa mikataba, machafuko ya kisiasa, na kuyumba kwa uchumi mkuu Hii humaanisha kwamba bara linakabiliwa na uwezekano wa kupoteza mitaji ambayo ni muhimu kwa kukuza uchumi, na kwa wawekezaj kukosa fursa za kugema kiwango kikubwa cha bidhaa/madini kutoka kwenye soko changa ambalo bado kwa sehemu kubwa halijashughulikiwa.

MIGA inaweza Kusaidia
MIGA inaweza kusaidia nchi za Kusini mwa Sahara kuvutia uwekezaji ambao hujenga ajira na kuchangia katika ukuaji uchumi na kusaidia wawekezaji kupata faida kutokana na mchakato huo. Jukumu la MIGA ni kusaidia ukuaji uchumi, kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu kwa kukuza uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja katika nchi zinazoendelea. Tunafanya hivyo kwa kutoa bima dhidi ya hatari za kisiasa (au wadhaminiwa), dhidi ya aina fulani za hatari ambazo si za kibiashara katika nchi zinazoendelea Ikiwa moja ya Taasisi mojawapo za Benki ya Dunia, MIGA iko katika nafasi nzuri zaidi ya kusaidia kutatua migogoro  ambayo inaweza kutokea baina ya wawekezaji na serikali za nchi mwenyeji MICA pia inafanya kazi kwa karibu na Benki ya Dunia na Shirika la Kimataifa la Fedha kuupa uwezo uwekezaji wa sekta binafsi, hususani katika miradi mikubwa ya miundombinu ambayo inahitajika kwa haraka zaidi ili kuweka misingi ya ukuaji uchumi.

MIGA haiweki kikomo cha ukubwa wa miradi inayosaidia Kwa uwekezaji mkubwa, MIGA inaweza kuhamasisha kiwango cha  udhamini unaohitajika



MIGA hutoa huduma za bima kwa uwekezaji wa  kigeni wa moja kwa moja dhidi ya hasara zinazohusiana na:
§  Zuio la kuhamisha na kubadilisha fedha za kigeni
§   Kutaifishwa kwa mali
§  Vita, fujo za raia, ugaidi na hujuma
§   Kuvunjika kwa mkataba
§  Kutokuheshimu masharti ya fedha ya nchi huru 

MIGA hutoa huduma za usuluhishi wa migogoro kwa uwekezaji uliodhaminiwa ili kuzuia kusambaratika kwa miradi



MIGA TAARIFA KWA MUHTASARI

Afrika Kusini mwa Sahara


                                                                                                                                                                                                                                                                     KUDHAMINI UWEKEZAJI   KUHAKIKISHA FURSA

MIGA katika nchi za Afrika Kusini mwa Sahara


  Bara linalopiga Hatua
Nchi za Bara la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara zimeendelea kuwa eneo linalo wavutia wawekezaji. Nchi hizi zimeshuhudia kuongezeka kwa kiwango cha juu na endelevu katika ukuaji wa uchumi katika miaka ya hivi karibuni, wakati makadirio yakionyesha kupanuka kwa uchumi kwa asilimia 5 kwa mwaka   2012, ikifuatia kupanuka kwingine kwa kiwango cha asilimia 4.7 mwaka 2011. Wakati sekta ya madini imekuwa ndio msukumo mkuu wa uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja katika bara hili, uwekezaji katika sekta ambazo si za uziduzi pia umekuwa ukiongezeka kutokana na maboresho ya taasisi za udhibiti, utawala bora na kwa ujumla mazingira mazuri ya kufanya biashara katika kanda hii—pia kuongezeka kwa tabaka la kati ambalo huvutia wawekezaji wanaotafuta masoko mapya.

Hisia za Hatari za Kisiasa Hukwamisha Uwekezaji uHH
Licha ya uwezo wake mkubwa, gharama za chini za nguvu kazi, na maliasili nyingi, wawekezaji wengi bado wanakuwa na wasiwasi wa kuwekeza katika bara la Afrika. Bara hili ni eneo lililo na nchi 17 ambazo Benki ya Dunia huzianisha kuwa ni nchi “tete na zilizogubikwa na migogoro”. Kwa baadhi ya wawekezaji, hatari za kufanya biashara katika nchi zilizo na usalama mdogo kisiasa mara nyingi ni kubwa zaidi kuliko faida ya kuingia masoko yenye faida kubwa. Na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara bado zinaonekana kuwa zina hatari kubwa, zenye gharama kubwa ya kufanya biashara. Hatari ambazo zinawapa wasiwasi wawekezaji na wakopeshaji mara nyingi zinahusiana na imani ndogo katika mfumo wa mahakama  

na taasisi za udhibiti, utawala mbovu, rushwa na uhaba wa utawala wa sheria, kutokuwepo kwa usimamizi wa mikataba, machafuko ya kisiasa, na kuyumba kwa uchumi mkuu Hii humaanisha kwamba bara linakabiliwa na uwezekano wa kupoteza mitaji ambayo ni muhimu kwa kukuza uchumi, na kwa wawekezaj kukosa fursa za kugema kiwango kikubwa cha bidhaa/madini kutoka kwenye soko changa ambalo bado kwa sehemu kubwa halijashughulikiwa.

MIGA inaweza Kusaidia
MIGA inaweza kusaidia nchi za Kusini mwa Sahara kuvutia uwekezaji ambao hujenga ajira na kuchangia katika ukuaji uchumi na kusaidia wawekezaji kupata faida kutokana na mchakato huo. Jukumu la MIGA ni kusaidia ukuaji uchumi, kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu kwa kukuza uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja katika nchi zinazoendelea. Tunafanya hivyo kwa kutoa bima dhidi ya hatari za kisiasa (au wadhaminiwa), dhidi ya aina fulani za hatari ambazo si za kibiashara katika nchi zinazoendelea Ikiwa moja ya Taasisi mojawapo za Benki ya Dunia, MIGA iko katika nafasi nzuri zaidi ya kusaidia kutatua migogoro  ambayo inaweza kutokea baina ya wawekezaji na serikali za nchi mwenyeji MICA pia inafanya kazi kwa karibu na Benki ya Dunia na Shirika la Kimataifa la Fedha kuupa uwezo uwekezaji wa sekta binafsi, hususani katika miradi mikubwa ya miundombinu ambayo inahitajika kwa haraka zaidi ili kuweka misingi ya ukuaji uchumi.

MIGA haiweki kikomo cha ukubwa wa miradi inayosaidia Kwa uwekezaji mkubwa, MIGA inaweza kuhamasisha kiwango cha  udhamini unaohitajika



MIGA hutoa huduma za bima kwa uwekezaji wa  kigeni wa moja kwa moja dhidi ya hasara zinazohusiana na:
§  Zuio la kuhamisha na kubadilisha fedha za kigeni
§   Kutaifishwa kwa mali
§  Vita, fujo za raia, ugaidi na hujuma
§   Kuvunjika kwa mkataba
§  Kutokuheshimu masharti ya fedha ya nchi huru 

MIGA hutoa huduma za usuluhishi wa migogoro kwa uwekezaji uliodhaminiwa ili kuzuia kusambaratika kwa miradi

No comments:

Post a Comment