Tuesday, June 12, 2012

JK awaapisha mabalozi wapya

MABALOZI wapya walioapishwa jana wameahidi kufanya kazi kwa bidii na kuendeleza ushirikiano kati ya Tanzania na nchi mbalimbali.Naimi Asizi (Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda), Dora Msechu (Mkrugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika), Ramadhan Mwinyi (Naibu balozi wa kudumu katika Umoja wa Mataifa)  na Irene Kasyanja (Mkurugenzi kitengo cha Sheria).

Wengine ni Vicent Kibwana (Mkurugenzi Idara ya Afrika), Celestin Mushy (Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa), Hassan Yahya (Mkurugenzi wa Mashariki ya Kati), Silima Kombo Haji (Mkurugenzi wa Mambo ya nje Zanzibar) na Mbelwa Kairuki (Mkurugenzi wa Asia na Australia).

Akizungumza baada ya hafla hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema hadi sasa kuna mabaliozi 32 walioko nje ya nchi na kwamba sasa wamefikia 42 na kwamba wamezingatia jinsia, umri na muungano katika kuteua mabalozi hao.



 Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete jana, mabalozi hao waliahidi kufanya kazi kwa ushirikiano.

Mmoja wa mabalozi hao, Naimi Asizi aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, alisema atahakikisha Tanzania inafanya vizuri katika Jumuiya mbalimbali kama za Afrika Mashariki, soko la pamoja (Comesa) na SADC.

Naye Balozi Dora Msechu alisema kuwa kuna changamoto nyingi za kukabiliana nazo kwa sasa hasa katika jumuiya mbalimbali hivyo atajitahidi kufanya kazi kwa bidii ili kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na nchi mbalimbali.

Naye balozi Bertha Somi ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Watanzania wanaoishi ughaibuni, alisema atafanya kazi kwa bidii na kuhakikisha Watanzania wanaoishi nje wanachangia maendeleo ya nchi.




 


No comments:

Post a Comment