Friday, June 29, 2012

Madaktari Haydom nao wagoma

Joseph Lyimo,Mbulu
MADAKTARI kumi wa Hospitali ya Haydom wilayani Mbulu katika Mkoa wa Manyara, wameungana na madaktari wa hospitali za Serikali nchini, katika mgomo wao unaondelea

Madaktari  wa hospitali hiyo ya rufaa inayotoa huduma zake kwa wagonjwa kutoka katika Mikoa ya Manyara na Singida, walianza kugoma juzi.Hatua hiyo imesababisha madaktari wengine wanaoendelea na kazi, kuelemewa na wingi wa wagonjwa.

 Hospitali hiyo ya Haydom, inamilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), lakini inapata vifaa tiba na dawa kutoka serikalini.Wakizungumza na waandishi wa habari kwa masharti ya kutotajwa majina, madaktari hao wanafanya masoma kwa vitendo katika hospitali hiyo, walisema hawataendea kutoa huduma hadi madai yao yatakapotimizwa.


Pia walilaani vikali tukio la kutekwa nyara na kujeruhiwa vibaya kwa Dk Ulimboka ."Hata hivyo sisi tunaendeleza mapambano ya kudai haki zetu kwa njia ya mgomo. Kwa nini wanatumia mbinu chafu za kijasusi  kushumghulikia Dk Ulimboka," alisema mmoja wa madaktari hao.

Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Anatory Choya, hatua ya madaktari katika Hospitali ya Haydom, kuingia katika mgomo.

Alisema hata hivyo, ofisi yake inaendelea na jitihada za kuzungumza nao, ili warejee kazini na kuwahudumia wananchi.

 Choya alisema kwa sasa madaktari wanaoendelea na kazi ,wameelemewa na mzigo wa kuhudumia idadi kubwa ya wagonjwa."Tulijaribu kuwaita ili tukae nao katika meza moja, lakini walikataa. Hata hivyo  tunamshukuru Mungu kwamba tangu walipogoma hakuna madhara yaliyotokea kwa wagonjwa waliopo hospitalini ," alisema Choya.


No comments:

Post a Comment