Umoja wa Mataiafa umesitisha shuguli za waangalizi wake nchini
Syria leo hii kutokana na kupamba moto kwa umwagaji damu wakati vikosi
vya serikali vikishambulia kwa mizinga ngome kuu za waasi.
mgogoro huo.
Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Susan Rice, amewafanananisha waangalizi hao na " watu wanaosubiri maafa bila ya kujitambuwa katika uwanja wa shabaha "
Akifafanuwa juu ya uamuzi huo, mkuu wa timu ya waangalizi hao, Meja Jenerali Robert Mood,
amezungumzia juu ya kupamba moto kwa mapigano, hatari inayowakabili waaangalizi hao 300 na halikadhalika kutokuwepo kwa nia ya kusuluhisha mzozo huo kwa njia ya amani kati ya pande mbili zinazohasimiana.
Siku 10 za mapigano
Amesema kimsingi mambo yanayotendekea nchini humo yanakwamisha uwezo wao wa kutekeleza shughuli zao kwa mujibu wa mamlaka waliyopewa.
Kwa mujibu wa Jenerali huyo, kukosekana kwa nia ya makundi husika kutafuta usuluhishi wa amani kwa mzozo huo na shinikizo la kuteka maeneo kunasababisha kuongezeka kwa maafa kwa pande zote mbili ambapo raia wasiokuwa na hatia, wanaume na wanawake halikadahalika watoto wanauwawa kila siku. Hali hiyo pia inawaweka katika hatari kubwa waangalizi wao.
Mood ameongeza kusema kwamba waaangalizi hao hawatopiga doria na watabakia kwenye vituo vyao hadi hapo itakapotolewa taarifa zaidi.
Kusitishwa kwa shughuli hizo za waangalizi wa Umoja wa Maataifa nchini Syria kutafanyiwa atahmnini kila siku na kwamba shughuli hizo zinaweza kuanza tena wakati hali itakaporuhusu kwa waangalizi hao kuweza kutekeleza shughuli zao kwa mujibu wa mamlaka yao.
Watu zaidi ya 30 wauawa
Zaidi ya watu 14,000 wameuwawa tokea kuanza kwa upinzani dhidi ya utawala wa Rais Bashar al-Assad hapo mwezi wa Machi 2011.
Kwa mujibu wa Rami Abdel Rahman wa Kituo cha Uangalizi wa Haki za Binaadamu nchini Syria katika mapigano ya umwagaji damu ya hivi karibuni kabisa, familia zimenasa kwenye mapigano hayo katika miji ya Khalidiyeh, Jourat al-Shiah, Qrabees na Qasoor - maeneo ya mji wa Homs ambao ni ngome kuu ya wapinzani.
Watu hao hawana chakula na hawapatiwi huduma za matibabu. Kituo hicho cha haki za binaadamu kimetowa wito wa daharura kwa Katibu Mkuu wa Mataifa, Ban Ki-moon, na wale wenye hisia ya ubinaadamu kuingilia kati katika kukomesha mashambulzi ya mizinga ya vikosi vya serikali.
No comments:
Post a Comment