Tuesday, April 23, 2013

UPELELEZI WA KESI YA WILFRED LWAKATARE PAMOJA NA LUDOVICK JOSEPH YAKAMILIKA


Jeshi la polisi nchini limefafanua juu ya hatua mbalimbali zilizofikiwa juu ya kesi mbalimbali nchini na kusema kuwa upelelezi wa kesi inayomkabili  bwana Wilfred Lwakatare pamoja na Ludovick Joseph umekamilika na jalada linaandaliwa kwenda  kwa mkurugenzi wa mashtaka (DPP) kwa hatua zaidi.

Matukio ambayo ameyatolewa ufafanuzi ni pamoja na matukio yaliyotokea Zanzibar,tukio la mhariri mtendaji wa habari ,bwana Absalom kibanda,Tukio la kumwagiwa tindikali  kada wa ccm bwana Musa Tesha katika uchaguzi mdogo na ubunge jimbo la Igunga mkoani Tabora septemba 2011,tukio la kutekwa na kuteswa kwa Dk.Ulimboka ,tuhuma za kuhusika na vitendo  vya kigaidi  zinazomkabili mkurugenzi wa  ulinzi na usalama wa chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA) Bwana Wilfred Rwakatare na  Ludovick Joseph pamoja na  matukio mengine mengi yaliyoripotiwa katika  vituo mbali mbali  vya polisi hapa nchini.

Akieleza kuhusu kesi ya kwamwagiwa Tindikali kada wa ccm bwana Mussa Tesha  katika  uchaguzi mdogo  wa Bunge jimbo la Igunga   mkoani Tabora septemba 2011;watuhumiwa wawili tayari wamefikishwa  mahakamani na upelelezi  upo katika hatua za mwisho,endapo watabainika watuhumiwa wengine nao watafikishwa mahakamani.

Kuhusiana na kesi ya kuvamiwa ,kupigwa nakujeruhiwa mhariri wa New habari 2006 ,bwana Absalom Kibanda,tukio la  kutekwa na kujeruhiwa  kwa Dkt .Ulimboka 'matukio yaliyotokea huko Zanzibar na matukio mengine yaliyoripotiwa katika vituo mbali mbali vya Polisi hapa nchini,uchunguzi wa matukio  haya bado unaendelea  na uko katika hatua  mbali mbali za kupelelezi ambazo kwa sasa si vema kuziweka wazi kuepusha kuharibu upelelezi unaoendelea.

Aidha kaimu mkurugenzi wa upepelezi wa makosa ya jinai nchini DCP Issaya Mngulu amewashukuru  wananchi  kwa ushirikiano wao mkubwa  unaosaidia kufanikisha upelelezi wa matukio ya uhalifu na hatimaye kufanikisha kukamatwa kwa wahalifu hapa nchini,pia amewaomba wananchi kuendelea na ushirikiano huo ili nchi yetu iendelee kuwa salama.

Mwisho DCP  Issaya Mngulu ameomba kufahamisha umma wa watanzania kwa ujumla kwamba zipo sheria na taratibu za kutoa habari na matukio yanayoripotiwa katika vituo vya polisi ,ieleweke wazi kuwa taarifa zinaporipotiwa vituoni kwa mujibu wa sheria  ni za siri kwa faida ya wahanga wa kesi na kwa ajili ya kufanikisha upelelezi wa kesi yenyewe ,aisha kanuni za jeshi la Polisi zinaruhusu kamanda  kutoa taarifa za tukio na sio kujadili ushahidi wa kesi ili kuepusha  kuadhiri mwenendo  mzima wa kesi ziwapo mahakamani.


Imetolewa na :
Issaya Mngulu DCP
kaimu mkurugenzi wa upelelezi makosa ya jinai nchini.   

No comments:

Post a Comment