Saturday, December 28, 2013

Aliyekuwa mchezaji wa zamani na Kocha wa makipa Simba, marehemu James Kisaka azikwa kwao Muheza Tanga


Jaji wa Mahakama ya Jumuia ya Afrika Mashariki (wa pili kulia na suti nyeusi), John Mkwawa akiuaga mwili wa marehemu James Kisaka leo, nyumbani kwao Muhenza, mkoani Tanga wakati wa shughuli za mazishi yake.
 Ndugu wakimlilia mpedwa wao, James Kisaka wakati wa mazishi yake Muheza, Tanga leo.
Padre wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Tanga, Mtaa wa Lusanga kwa Yesu, akitoa maneo ya kuagwa kwa mwili wa marehemu James Kisaka, wakati wa mazishi yake leo.
 Padri wa Kanisa la Anglican, Aidano Kamote akiuaga mwili wa James Kisaka.
Waombolezaji wakishirikiana kuuingiza kaburini mwili wa marehemu James Kisaka, wakati wa mazishi yake, Muheza Tanga.
Wapenzi wa mchezo wa pira wa miguuu, Juma Mgunda wa Coastal Union (kulia) na mwenzake ambaye jina lake halikuweza kupatikana, wakiwa wanaonekana na huzuni kufuatia kifo cha aliyekuwa mchezaji mwenzao, wakati wa miaka ya 1980, James Kisaka aliyedakia Simba na kisha kuwa kocha wa makipa wa timu hiyo hivi karibuni. (Picha zote na Dotto Mwaibale)

No comments:

Post a Comment