Sunday, March 2, 2014

Mwenyekiti wa Chadema ahamia CCM

*Atoa mazito ya moyoni.

*Ahidi kukimaliza chama hicho katika uchaguzi Jimbo la Kalenga

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kata ya Nzihi akijitambulisha rasmi kwa wananchi wa Kijiji cha Nzihi kuwa yeye ameamua kuachana na chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa hiari yake, baada ya kupima uwezo wa chama hicho na CCM katika Hoja na Matendo.

Mwanachama huyu mpya wa CCM, ameahidi kuongoza timu ya ushindi ya chama hicho, kwenye Kata ya Nzihi kuhakikisha mgombea wake, Godfrey Mgimwa anapita kuwa Mbunge.

Pia amesema kuwa ataiweka wazi mipango ya chama chake cha zamani (Chadema) na watu wageni wa Chadema waliokodishwa na kupangishiwa nyumba katika Kata ya Nzihi, wanaotembea usiku kwa ajili ya kutafuta kura na kushambulia waowaunga mkono CCM kwenye Kata ya Nzihi.

Mwingine alijiunga na CCM ni kutoka Kijiji cha Kamiyu na ambaye ni Katibu Mwenezi wa Chadema Kata ya Kamiyu aliyetangaza kuachana na Chadema na Kujiunga na CCM hii leo kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Nzihi. (Na Richard Mwaikenda wa Kamanda wa Matukio Blog)

No comments:

Post a Comment