Monday, August 25, 2014

Jinsi MIGA inavyofanya kazi


MIGA
Taasisi ya Kudhamini Uwekezaji
 TAASISI ZA BENKI YA DUNIA
Taarifa kwa Vyombo vya Habari


Mfano wa Maelezo Mafupi ya Mradi
Muhtasari wa mapendekezo ya udhamini hutolewa kabla ya vikao vya maamuzi ya Bodi na kabla ya hatua ya mwisho ya kusaini mkataba, hivyo huweza kubadilishwa. Muhtasari wa taarifa za mradi huwekwa bayana baada ya maamuzi ya Bodi na kusainiwa kwa mkataba, na huakisi vigezo vinavyoambatana na mradi wakati wa kusainiwa mkataba. Muhtasari wa Mapitio ya Athari za Kimazingira na Kijamii hutolewa kwa miradi ambayo imeainishwa katika Kundi A au B la Tathmini ya Athari za Mazingira.
Jina la Mradi:                        Kahama Mining Corp. Ltd.
Utambulisho wa mradi:        3661
Mwaka wa fedha:                 2001
Hadhi ya mradi:                    Haufanyi kazi
Mdhamini:                             Kampuni ya Barrick Gold Corp. ya Canada
Nchi ya mwekezaji:               Canada
Nchi ya uwekezaji:                Tanzania
Sekta:                                                 Madini
Thamani kuu ya mradi:       Dola za Marekani milioni 56.2  
Aina ya Mradi:                      Non-SIP
Mdhaminiwa mpya wa MIGA atasaidia kutumia rasilimali ambazo hazijaendelezwa za sekta ya madini nchini Tanzania, hivyo kusaidia nchi kupanua wigo wake wa uchumi. Katika mwaka wa fedha 2001, Kampuni ya Barrick Gold Corp. ya Canada ilipokea udhamini wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 56.25 kutoka MIGA kwa ajili ya uwekezaji kwenye mgodi wa dhahabu, fedha, na shaba nchini  Tanzania. Kampuni binafsi za bima zinatoa uhakikisho wa udhamini wa uwekezaji huu. Bima hii itakinga uwekezaji dhidi ya hatari za zuio la kuhamisha faida, kutaifishwa kwa mali, madhara ya vita na fujo miongoni mwa raia. Shirika la Maendeleo ya Bidhaa Nje la Canada pia ni mdhamini katika mradi huu.
Mradi unahusisha kuanzishwa na kuendesha mgodi na mitambo yake. Katika uhai wa mgodi, mradi unatarajiwa kuzalisha kila mwaka wakia 420,000 za dhahabu, wakia 240,000 za fedha, na kilo milioni 3.8 za shaba. Mbinu bunifu zinatumika kuondoa mabaki ya uzalishaji, kutumia teknolojia ya kugandisha madini na kujaza mashimo ya mgodi.
Uwekezaji utachangia katika maendeleo ya miundombinu ya nchi. Jamii zinazonguka mgodi zitanufaika moja kwa moja kwa kupata maji kutoka kwenye mabomba yanayojengwa na wafadhili wa mradi, upatikanaji wa umeme kwa kaya za wanavijiji, na maendeleo ya barabara.
Mradi utatengeneza takribani ajira 1,500 wakati wa ujenzi na zaidi ya ajira mpya 1,000 za kuendesha mgodi. Chini ya makubaliano na serikali, mradi utatayarisha na kutekeleza programu ya ajira na mafunzo kwa wafanyakazi wake wa Kitanzania katika kila awamu na katika ngazi zote za kuendesha mradi. Mradi utalipa takribani Dola za Marekani milioni 75 kama kodi, mrahaba na ushuru kwa serikali wakati wa miaka yake 15 ya mwanzo, na kununua bidhaa na huduma zinazozalishwa nchini zenye thamani ya takribani Dola za Marekani milioni 10.  

No comments:

Post a Comment