Tuesday, August 5, 2014

MTU MMOJA ASHIKILIWA KWA KUKUTWA NA NGOZI YA CHUI KINYUME CHA SHERIA


Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linamshikilia mtu mmoja VENANCE S/O MANYIKA, Miaka 38, Mkazi wa Mbagala Massion kwa kosa la kukutwa na ngozi ya chui kinyume cha sheria.

  Mtuhumiwa huyu alikamatwa tarehe 29/07/2014 huko Mbagala Mission na askari waliokuwa katika misako inayoendelea yenye lengo la kupambana na uhalifu jijini Dar es Salaam. 

 Wakiwa katika misako hiyo Polisi walipokea taarifa kuwa kuna mtu wanayemuhisi kujihusisha na uuzaji wa nyara za Serikali ndipo walipofika eneo la tukio na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa. 


Upelelezi wa shauri hili unaendelea na jalada la mtuhumiwa litapelekwa kwa mwanasheria wa Serikali ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

S. H. KOVA,
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM


No comments:

Post a Comment