Sunday, August 24, 2014

WATU SABA WAKAMATWA KWA KUJIHUSISHA NA UTENGENEZAJI WA NOTI BANDIA ZA DOLA ZA KIMAREKANI WAKAMATWA




      Jeshi  la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limefanikiwa kukamata kundi la watu saba wanaotengeneza noti bandia za Dolla ya Kimarekani huko maeneo ya Sinza katika Hotel iitwayo Mombasa Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Watuhumiwa hao walikamatwa mnamo tarehe 04/8/2014 wakiwa na noti bandia zipatazo 10,640 za dola mia (100) ambazo ni sawa na DOLLA 1,064,000 (Dolla Millioni Moja na Sitini na Nne Elfu) sawa na shilingi za kitanzania 1,702,400,000/= (TSH. Billioni Moja, Millioni Mia Saba na Mbili na Laki Nne) katika nyumba namba 07 walimokuwa wamepanga.
Polisi walipata taarifa toka kwa wasamaria wema na kuweka mtego wa kuwakamata ndipo askari walipofika eneo hilo waliwakamata watuhumiwa na noti za USD bandi zikiwa zimefungwa mabunda themanini na kasiki ndogo ambayo imefungwa kwa namba za siri. 
    Aidha watuhumiwa hao walikiri kujihusisha na utengenezaji wa noti bandia, watuhumiwa hao ni kama ifuatavyo;
1.AHMAD S/O MOHAMED Miaka 50, mfanyabiashara, mkazi wa Mombasa Kenya
2.ICHARD S/O MAGOTI Miaka 61, mfanyabiashara, mkazi wa Musoma mkoani Mara.
3.SIMONI S/O LUKIKO Miaka 58, mkazi wa Magomeni Kagera
4.HUMPREY S/O LEONARD Miaka 34, mlinzi, mkazi wa Mburahati
5.FRANK S/O CHARLES Miaka 31 mfanyabiashara, mkazi wa Sinza
6.ABDALLAH S/O YUSUPH,  Miaka 34, mfanyabiashara, Mkazi wa Sinza
7.BAKARI S/O BAKARI,  Miaka 31, mfanyabiashara, mkazi wa Mbezi, Kimara.
Aidha watuhumiwa hao wanaendelea kuhojiwa na upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

KUPATIKANA KWA BHANG GUNIA TATU (3), GONGO LITA 600 NA WATUHUMIWA
Aidha katika tukio lingine Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limeendelea kufanya operesheni na limefanikiwa kukamata watuhumiwa watano wakiwa na gunia tatu za dawa za kulevya aina ya Bhang na Gongo lita 600 na mitambo sita ya kutengenezea pombe hiyo haramu ya Moshi

No comments:

Post a Comment